CHADEMA Kumshtaki Dr. J.Pombe Magufuli anayewania Uraisi kwa tiketi ya Chama cha CCM.
CHAMA
cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimepanga kumshitaki mgombea wa
urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. John Magufuli kwa madai ya
kutumia vibaya nembo za chama hicho.
Ni
baada ya Dk. Magufuli kutangaza kuwa nembo ya Movement for Change (M4C)
ni Magufuli For Change wakati akifanya mkutano wake wa kampeni mkoani
Kigoma kwenye Uwanja wa Kawawa uliopo Ujiji.
Katika mkutano huo Dk. Magufuli alisema “hawa jamaa zangu wa Chadema wananipenda, hata ile nembo yao ya M4C ni Magufuli for Change-maana yake Magufuli kwa Mabadiliko.”
Chadema
wanaratajia kufungua kesi hiyo Septemba 21 mwaka huu na kwamba, madai
hayo yatakwenda sambamba na madai ya kutumia kauli mbiu
Akizungumza
na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam katika Ukumbi wa Ngome
Kawe, Mwanasheria wa Chadema, John Malya alisema “CCM imekuwa
ikivunja sheria za uchaguzi kila siku bila kuchukuliwa hatua yoyote na
mamlaka husika, wanatumia nembo za Chadema ambazo zimesajiliwa na
kujulikana.”
Hata
hivyo imeelezwa, baada ya Dk. Magufuli ‘kuiba’ alama hizo za Chadema;
wafuasi wake, bodi ya wadhamini na watu wake wa kampeni walianza
kusambaza mitandaoni nembo ya M4C huku wakidai ni nembo mpya ya CCM.
Malya
alisema mbali na hilo la kuiba nembo ya chama, wamekuwa na tabia ya
‘kukopi’ na ‘kupesti’ kila hatua inayo pigwa na Chadema na kuzitumia
katika kampeni zao.

No comments:
Post a Comment