Sunday, August 2, 2015

Mchungaji Mtikila akichukua fomu ya Uraisi kwa kuzua lingine Tata.

Mwenyekiti wa Democratic Party (DP), Mchungaji Christopher Mtikila  akisaini nyaraka za Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec) za kuthibitisha kupokea fomu za kugombea Urais  zilizokabidhiwa na Ofisa Mwandamizi wa Tume  hiyo George Kashura jijini Dar es Salaam
Mchungaji Mtikila ambaye aliambatana na mgombea mwenza Juma Metu Juma, alitaka ufafanuzi wa kutokuruhusiwa kuwania urais akiwa mgombea binafsi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati Mahakama ya Haki za Binadamu ya Afrika (AfCHPR) imeruhusu.


Mchungaji Mtikila ambaye aliambatana na mgombea mwenza Juma Metu Juma, alitaka ufafanuzi wa kutokuruhusiwa kuwania urais akiwa mgombea binafsi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati Mahakama ya Haki za Binadamu ya Afrika (AfCHPR) imeruhusu.
“Siondoki hapa na wala sitaweza kuchukua hizi fomu hadi mniambie ni wapi nitapata jibu la tume la kukiuka maagizo ya mahakama ya Afrika.
“Waandishi embu subirini kwanza mkurugenzi wa uchaguzi aje hapa ilia atoe ufafanuzi na nyie msikilize mkaandike ukweli kwa sababu hii siyo haki ni sawa na kudharau mahakama,” alisema.
Baada ya kuzozana na maofisa waliokuwa wakimkabidhi fomu hizo, walilazimika kumuita mkurugenzi wa uchaguzi Kailima Ramadhani, ambaye alimwambia kwamba sheria hairuhusu.
“Sisi tunafuata sheria mwenyekiti kama hicho kipengele kingekuwapo tungekuruhusu uchukue fomu hizo, lakini hapa tunabanwa na sheria tunaruhusu kutoa fomu kwa watu wanaotoka kwenye vyama vyao,” alisema Ramadhani.

No comments: